Mbulu is a town in Tanzania and the capital of the Mbulu District. The town is inhabited by people that identify as Iraqw people. The Roman Catholic Diocese of Mbulu is also located in Mbulu.
Mbulu also (known as Imboru among the Iraqw speakers) is the town in Northern Tanzania. The town is the core of minority cushitic speakers (iraqw people) in Tanzania. The town was founded by Germans in 1907 when they colonizes former German East Africa (Tanganyika, Burundi and Rwanda). Mbulu climate favoured Germans, also the hospitality of the indigenous favoured them. Germans were less harsh to the Iraqw people than the rest Tanganyikans. Thus Iraqw were used by Germans on white collar jobs. Today most Afro-German with Tanzanian ancestry are Iraqw from Mbulu. The main economic activities in Mbulu are Agriculture and Trade. Mbulu area is one of the earliest Wheat growing Plantations. During the British regime, Mbulu peasants were able to form trade union, Particularly Mbulu Wheat Growers association (1923). Most Famous people born in Mbulu are:
RAMANI YA WILAYA YA MBULU KUOYESHA MIPAKA TUNAYOPAKANA NAYO.
	

	
	
	
	
	
CHIMBUKO LA WAIRAQ!
	
 WAIRAQ au Wairaki ni kabila kubwa
	
 linalozungumza lugha jamii ya Wakushi na
	
 linalopatikana Mkoa wa Manyara wilaya za
	
 Mbulu, Babati, Hanang na Mkoa wa Arusha
	
 katika wilaya ya Karatu.
	
 Watu wa kabila hilo wanauhusiano wa asili na
	
 makabila ya Gorowa, Burungi na Alawa ambao
	
 wanaishi katika wilaya za Babati na Kondoa.
	
 Historia kwa njia ya simulizi za makabila inasema
	
 chimbuko la Wairaqw linatokana na kizazi cha
	
 watu wa kale walivyokuwa wakiishi eneo la
	
 Mesopotamia, Iraq.
	
 Vita ya mara kwa mara ilisababisha watu hao
	
 kuhama makazi yao ya asili katika karne ya nne
	
 hadi ya sita baada ya kuzaliwa kwa Kristo.
	
 Wairaqw walivuka bahari ya Sham kwa mashua
	
 na kutua Ethiopia ambako waliishi kwa muda
	
 kisha kuendelea kuhama kuelekea Kusini
	
 Magharibi kupitia bonde la ufa kando ya Ziwa
	
 Victoria na kuweka kambi eneo waliloona ni
	
 salama.
	
 Kwa kuwa ni watu wasiopenda vita waliendelea
	
 kuhamahama wakikimbia vita vilivyoruka sehemu
	
 mbalimbali walizojaribu kuweka kambi. Walipita
	
 njia ya kati kupitia Iramba Mkoa wa Singida
	
 Iramba hadi mpakani mwa Dodoma na Iringa
	
 ambapo walikutana na mapambano ya Wahehe,
	
 Wangoni na Wazimba.
	
 Hali hiyo iliwalazimu kubadilisha njia na kurejea
	
 kuelekea Kaskazini hadi sehemu ya Kondoa
	
 mahali panapoitwa Guser Tuwalay na kuishi eneo
	
 hilo huku wakijishughulisha na ufugaji na kilimo
	
 kidogo. Hata hivyo ilitokea kutokuelewana kati
	
 yao na watu wa kabila la Wabarbaig jambo
	
 lililosababisha vita.
	
 Ingawa walikuwa waoga wa vita walikuwa na
	
 silaha za kujihami dhidi ya vita. Walitumia mikuki
	
 na mishale ya asili ilitengenezwa na miti
	
 iliyochongwa mfano wa mkuki wa chuma
	
 unaotumika sasa. Pia walitumia mawe yenye
	
 ncha kali na baadaye waligundua zana
	
 zinazotengenezwa kwa kutumia udongo wa
	
 mfinyanzi ambazo zilikaushwa kwa moto mkali
	
 kama tofali.
	
 Hata hivyo Wairaq walishindwa vita na kukimbilia
	
 karibu na mlima Hanang kisha wakagawanyika
	
 wengine wakaelekea mlima Dabil hadi Guser na
	
 Gangaru ambapo walifanya maskani. Wairaq
	
 walikuwa na uongozi toka ngazi ya familia, ukoo,
	
	
	
	
	
	
	
	
ASILI YA JINA LA MBULU
	 
	 
	 Alfredo is with Philomena Buxay and 13 others.January 19
Alfredo is with Philomena Buxay and 13 others.January 19
	
	
NINI ASILI YA JINA MBULU? IJUE HISTORIA YA JINA MBULU SASA!
Wakati Wairaqw wakiwa bado wanakaa ``Irqwar Da/aw`` yaani bado hata hawajaanza kuhamia maeneo ya Mbulu, kuna binti alikuwa anaitwa Imbori alipata mimba yaani Doroway.
Doroway ilikuwa inaleta unajisi ``meeta`` kwenye familia husika na katu binti hakuruhusiwa kuzaa nyumbani na hawezi kuolewa na Mwiraqw yeyote, hivyo ilibidi Imbori afukuzwe kwao salama yake ni aolewe na mtu wa kabila lingine yaani ``homo`` ambao mara nyingi ni wadatoga au wambugwe.
Lakini kulikuwa na taratibu za kufuata na ilikuwa hivyo pia kwa Imbori. Alipobainika anamimba, Imbori alinyolewa nywele na kupakwa majivu kichwani ikiwa ni utambulisho kuwa ana``doroway`` alipfungashiwa chakula ambacho mara nyingi huwa viazi au mahindi ya kuchoma (haya yalikwepo muda wote kutokana na hali ya hewa ya Irqwar Da/aw) na kuongozwa na kaka yake aliyekuwa anatembea mbele yake ili amkabidhi kwa ``homo`` yeyote atakayejitokeza kama anataka mke au chakula kikiisha afie hukohuko porini au aliwe na wanyama.
Wakafika sehemu inayoitwa Mantla ambapo ni njia panda moja inaelekea Murray na nyingine Kainam na kwa kuwa Nade Be/a ambaye ni mganga maarufu kutoka Manda do Bayo alikuwa anakaa Murray hawakuthubutu kupitia njia hiyo maarufu kama ``tlo/u /awaak`` ambayo pia ilikuwa njia ya wamasai waliokuwa tishio kwa wairaqw hivyo wakapita njia ya Kainam hadi Aya Ma/ami ambako alifanikiwa kumpata ``homo`` aliyemwoa akaondoka naye hadi Mbulu.
Alipokwisha kuolewa ile ``meeta`` ikaisha na ndipo ndugu zake (pengine hata yeye mwenyewe baadaye) kumfuatilia kwa njia aliyofuatana na huyo mume wake na kufanikiwa kumpata na hatimaye kumtembelea mara kwa mara.
Katika kumtembelea huko, walikuwa wakisema tunaenda kwa Imbori ``do imboru kawaan``na hatimaye pakawa maarufu kama kwa Imboru na hatimaye Imboru.
 Wajerumani walipofika wakashindwa kutamka Imboru wakawa wanasema Mbulu na ndipo hatimaye jina Mbulu likawa ``official``
	
 Ahsanteni!
	
	
	
	

	
	
 
  
          
                              
                              
                            Mbulu district Coucil
Anuani: P.O.BOX 74
Simu ya mezani: +255743583078
Simu: +255716992222
Barua pepe: md@mbuludc.go.tz
Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.