• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Dinamu
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

NAFANYAJE KUPATA LESENI YA VILEO

Utaratibu wa kupata Leseni za Vileo

Sheria ya leseni za vileo imenyambulisha aina tisa za leseni za vileo zinazoweza kutolewa chini ya sheria hii: Retailers On Leseni hii humruhusu mwenye biashara kuuza pombe na kunywa eneo la biashara RETAILERS OFF Leseni hii haimruhusu mtu kinywea pombe eneo la biashara bali kwa watu wanaochukua kunyewea majumbani (Take away) kama Groceries. WHOLESALE Leseni hii ni kuuza pombe kwa jumla HOTEL Leseni hii humruhusu mwenye leseni kuuza pombe kwa ajili ya kunywea katika eneo la biashara kwa watu waliopanga hotelini kwa wakati wowote wa mchana na usiku RESTAURANT. Leseni hii inamruhusu mwenye leseni kuuza pombe kwa mtu yeyote anayekula chakula katika mgahawa katika muda wa saa 6.00 mchana hadi saa 8.00 mchana na saa 12.00 hadi saa 6.00 usiku.

MEMBERS CLUB Leseni hii huruhusu uuzaji wa pombe kwa kiasi chochote kwa mwanachama wa Klabu na wageni wao tu COMBINED Leseni ambazo zimeambatanishwa mbili kwa pamoja: (a) Combined Hotel and retailers on (b) Combined Hotel and Restaurant (c) Combined restaurant and retailers on TEMPORARY Leseni hii humruhusu mwenye leseni kuuza pombe katika sehemu iliyotajwa kwenye leseni mahali penye burudani, starehe au mkusanyiko mwingine kwa kipindi kisichozidi siku tatu LOCAL LIQUOR Class A Local Liquor Leseni hii humruhusu mwenye leseni kutengeneza pombe za kienyeji katika sehemu iliyotajwa na kuuza kwa ajili ya kunywea sehemu ya biashara au nje ya sehemu ya biashara.

Class B Local Liquor Leseni hii humruhusu kutengeneza pombe ya kienyeji sehemu iliyotajwa na kwenda kuuzia sehemu nyingine iliyo na leseni ya kuuza pombe za kienyeji Class C Local Liquor Leseni hii humruhusu kutengeneza pombe ya kienyeji katika sehemu iliyotajwa kwenye leseni na kuuza kwa mwenye class D au Class E Class D Local Liquor Leseni hii humruhusu kuuza pombe za kienyeji katika sehemu iliyotajwa kwenye leseni kwa kunywea eneo la biashara Class E Local Liquor Leseni hii humruhusu kuuza pombe za kienyeji kwa ajili ya kunyewea sehemu nyingine mbali ya eneo la biashara

1. MASHARTI YA KUPATA LESENI Mtu yeyote raia wa Tanzania anayo haki ya kupatiwa leseni ya Vileo ili mradi awe ametimiza umri wa miaka kumi na nane (18) mwenye akili timamu ambaye hajawahi kupatikana na kosa la jinai na awe na eneo la kufanyia biashara linalokubalika kisheria. Kwa mtu ambaye sio raia wa Tanzania anapaswa kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya biashara nchini kutoka Idara ya Uhamiaji.

2. UTARATIBU WA KUPATA LESENI • Mwombaji hujaza fomu za maombi zinazotolewa na Manispaa • Eneo/jengo linalokusudiwa kufanyia biashara hiyo kukaguliwa na Afisa Afya, Afisa Mipangomiji, Polisi, Afisa Mtendaji wa Kata na Afisa Biashara wa Halmashauri na hutoa maoni yao kwenye fomu husika • Maombi hayo hupelekwa katika Malaka ya Utoaji wa Leseni za Vileo ya Wilaya kwa uamuzi • Mwombaji ambaye maombi yake yamepitishwa hupewa Leseni baada ya kulipa ada inayotakiwa na ni lazima amekamilisha masharti ya kupata leseni hapo juu.

VIWANGO VYA ADA Viwango vya ada vinavyotumika kwa sasa kwa aina mbalimbali za leseni ni kama zifuatavyo:- 1. Retailers On (Baa) - 30,000.00 hadi 40,000.00 2. Retailers Off (Grosari) - 20,000.00 hadi 30,000.00 3. Wholesale (Jumla) - 10,000.00 hadi 20,000.00 4. Members Club (Klabu Wanachama) - 10,000.00 hadi 20,000.00 5. Restaurant & Retailers On - 30,000.00 hadi 40,000.00 6. Temporary licence (Leseni ya muda) - 7,000.00 hadi 15,000.00 7. Hotel Licence (Leseni ya Hoteli) - 30,000.00 hadi 40,000.00 8. Retailers Off non-spirituous - 7,000.00 hadi 15,000.00 9. Retailers On – non-spirituous - 10,000.00 hadi 15,000.00 Mamlaka ya Vileo itaamua kiwango cha ada kitakachotozwa kati ya kiwango cha chini na kile cha kima cha juu. Viwango vinavyotumika kwa sasa na Halmashauri ni vile vya kima cha juu kwa kila aina ya leseni.

3. MASHARTI YA UTUMIAJI Leseni za vileo zina masharti mengi ikiwa ni pamoja na kutouza kilevi kwa watoto. Masharti mengine ni muda wa kuuza pombe na kelele za muziki. MUDA WA KUUZA POMBE BAA (RETAILERS ON) • Jumatatu hadi Ijumaa - Saa 12.00 jioni hadi saa 5.00 Usiku • Jumamosi, Jumapili na Sikukuu - Saa 5.00 asubuhi hadi saa 8.00 mchana na saa 12.00 jioni hadi saa 6.00 usiku GROSARI (RETAILERS OFF) • Jumatatu hadi Ijumaa - Saa 2.00 asubuhi hadi saa 1.00 jioni • Jumamosi, Jumapili na Sikukuu - Saa 3.00 asubuhi hadi saa 6.00 mchana RESTAURANT LICENCE (MGAHAWA) • Jumatatu hadi Ijumaa - Saa 6.00 mchana hadi saa 8.00 mchana na saa 12.00 jioni hasi saa 6.00 usiku • Jumamosi, Jumapili na Sikukuu - Saa 5.00 asubuhi hadi saa 8.00 mchana na saa 12.00 jioni hadi saa 6.00 usiku MAKOSA Baadhi ya makosa chini ya sheria hii: •

Kuruhusu biashara nyingine isiyokubalika kisheria kufanyika eneo la biashara • Kuuza pombe kwa mtu mwenye umri chini ya miaka kumi na sita (16) • Kuajiri mtu chini ya miaka kumi na sita (16) kuuza pombe • Kuruhusu mtu mwenye umri chini ya miaka kumi na sita kukaa eneo la kuuzia pombe • Kutoweka leseni sehemu ya wazi, ambapo itaonekana kwa urahisi na wakaguzi • Kumruhusu/kuleta fujo katika eneo la biashara • Kuruhusu eneo la biashara kutumika kama danguro • Kuuza pombe muda ambao ni kinyume cha sheria • Kufanya biashara ya pombe kwa kutumia leseni ya vileo ambao haistahili ADHABU Mfanyabiashara anayetenda mojawapo ya makosa haya akikamatwa, atafikishwa mahakamani na akitiwa hatiani atalipa faini au kifungo au adhabu zote kwa pamoja.

Matangazo

  • Tangazo la fursa za mafunzo ya ufundi stadi awamu ya saba February 01, 2025
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • JINSI YA KUTOA/KUTUMA MALALAMIKO KWA NJIA YA MTANDO HALMSHAURI YA WILAYA YA MBULU. March 23, 2019
  • KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU 2021 June 10, 2021
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • MADIWANI WAPONGEZWA KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI KATIKA KATA ZAO

    April 29, 2025
  • MBULU DC YATOA SADAKA KITUO CHA AFYA DONGOBESH.

    January 30, 2025
  • MBULU DC YAKWAMUA VIKUNDI VYA VIJANA KIUCHUMI

    February 13, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 38.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 13, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

MBULU DC KUKUSANYA ZAIDI YA MIL.90 KATIKA MSIMU MPYA WA UVUVI KUTOKA BWAWA LA BONDELA YAEDA CHINI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.