• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Dinamu
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

UCRT YAZINDUA MRADI WA UHIFADHI JUMUISHI WA MAZINGIRA NA KUBORESHA MAISHA YA JAMII YA MBULU.

Kurushwa hewani: March 20th, 2024


Na Ruth Kyelula, Mbulu DC,

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbulu, Paulo Bura ambaye amemwakilisha mkuu wa Wilaya ya Mbulu Veronica Kessy, amewataka watendaji wa vijiji, wenyeviti wa vijiji na watendaji wengine wa kata waweze kuwapa ushirikiano wa kila hali shirika la UCRT ili kile walichokuja nacho kiweze kuwanufaisha wananchi wa wilaya ya Mbulu na lengo lao la makusudi na nia yao njema iweze kutimia.

Hayo yalisemwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Mbulu, Paulo Bura, wakati akifungua kikao cha uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa Mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa vijiji sita, chini ya Ujamaa Community Resource Team (UCRT), uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu Machi 19, 2024.

Picha ya pamoja ya meza kuu na watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Mbulu wakati wa uzinduzi wa mradi wa UCRT.

“Lakini sisi tulioingia kwenye awamu hii vijiji hivi sita, pia tujue sisi ni mfano wa vijiji vingine ambavyo vimeendelea kuombwa ili viingie kwenye mradi,wale wa awamu ya kwanza vijiji vitano hawajatuangusha,ndio maana maombi yalivyorudishwa kwa wahisani wa maendeleo wakaona vile vijiji vilifanya vizuri, kwahiyo hata hivi vijiji sita vikifanya vizuri vinaweza kuwa fursa na mlango kwa ajili ya vijiji vingine, kwa hiyo sisi ambao tuliopata fursa na bahati hiyo tuweze kuitumia vizuri ili basi tuweze kufungua milango kwa vijiji vingine kuweza kunufaika na mradi huu mzuri kwa ajili ya hifadhi ya mazingira lakini pia kwa ajili ya uchumi wa wananchi wetu.” Alisema Bura.

Viongozi wa vijiji na kata ambao ni wanufaika wa mradi.

Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa Hamashauri ya wilaya ya Mbulu Petro Tarmo aliwaomba wale wanufaika wa mradi wa zamani waendelee kutoa ushirikiano na hawa wapya waendelee pia kutoa ushirikiano kwa UCRT, waendelee kutoa elimu kwa wananchi na kuepuka migogoro ya mipaka ambayo inaweza kupelekea changamoto kwenye mradi. Waepukane na migogoro ili waende kwenye maslahi mapana ya wananchi. Aidha mratibu wa Ujamaa Community Resource Team (UCRT), Dismas Meitaya ameushukuru uongozi wa wilaya Mbulu kwa ujumla kwa kuweza kuushirikiana nao vizuri kwa Zaidi ya miaka ishirini waliyokuwa wakitekeleza miradi yao. Ikiwemo ofisi ya mkuu wa Wilaya, ofisi ya Mkurugenzi, wataalam wa hamashauri na viongozi wa vijiji.

Viongozi wa vijiji na kata ambao ni wanufaika wa mradi.

Alisema kuwa malengo makuu ya UCRT ni kuwezesha jamii ya asili kuweza kumiliki, kusimamia na kunufaika na ardhi. Na wamelenga Zaidi kwenye jamii ya wakusanya matunda, ambao ni wa hadzabe na waakie, wamaasai, wadatoga pamoja na wafugaji – wakulima wabatemi na wa iraqw.


Watuumishi wa Halmashauri wakifuatilia kwa umakini ufunguzi wa mradi wa awamu ya pili wa UCRT.

“Huu mpango ni shirikishi sana, wakina mama wanapewa kipaumbele na washiriki kisawa sawa. Kwa hiyo nataka kuona jamii ya akina mama na vikundi vingine wakiwa mstari wa mbele kushirikishwa kwa kila hatua ambayo tunakuja kufanya.” Alisema Dismas.

Alibainisha vijiji lengwa sita vya mradi katika bonde la Yaeda na ziwa Eyasi ni Garbabi, Yaedakati, Dirim, Endalat, Murkuchida na Endamilay.

Matangazo

  • Tangazo la fursa za mafunzo ya ufundi stadi awamu ya saba February 01, 2025
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • JINSI YA KUTOA/KUTUMA MALALAMIKO KWA NJIA YA MTANDO HALMSHAURI YA WILAYA YA MBULU. March 23, 2019
  • KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU 2021 June 10, 2021
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • MBULU DC YATOA SADAKA KITUO CHA AFYA DONGOBESH.

    January 30, 2025
  • MBULU DC YAKWAMUA VIKUNDI VYA VIJANA KIUCHUMI

    February 13, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 38.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZA WANAFUNZI WARIPOTI SHULENI

    January 31, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

MBULU DC KUKUSANYA ZAIDI YA MIL.90 KATIKA MSIMU MPYA WA UVUVI KUTOKA BWAWA LA BONDELA YAEDA CHINI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.