• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • WAHESHIMIWA MADIWANI
    • MADIWANI VITI MAALUM
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

USHIRIKIANO WA KITENGO CHA USTAWI WA JAMII NA TAASISI YA CHaRA WAWEZESHA WANAFUNZI WA KIKE DONGOBESH SEKONDARI KUPITIA ELIMU YA AFYA, KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA NA UGAWAJI WA TAULO ZA KIKE

Kurushwa hewani: February 9th, 2026

Kitengo cha Ustawi wa Jamii kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu kwa kushirikiana na Taasisi ya CHaRA imefanikiwa kutoa elimu ya afya kwa wanafunzi wa kike wa Shule ya Sekondari Dongobesh, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha ustawi, ulinzi na maendeleo ya mtoto wa kike katika jamii.


Elimu iliyotolewa ilijikita katika masuala ya afya ya uzazi na hedhi salama, madhara ya ukatili wa kijinsia pamoja na namna ya kujilinda na kutoa taarifa pindi vitendo vya ukatili vinapotokea. Kupitia mafunzo hayo, wanafunzi walipata fursa ya kuuliza maswali, kushirikishwa uzoefu na kupewa maarifa yatakayowawezesha kufanya maamuzi sahihi yanayohusu afya na maisha yao kwa ujumla.


Aidha, katika tukio hilo wanafunzi wa kike waligawiwa taulo za kike kama sehemu ya kusaidia wasichana kuhudhuria masomo yao kwa uhakika, kuongeza kujiamini na kupunguza changamoto zinazotokana na ukosefu wa vifaa vya kujisitiri wakati wa hedhi.


Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Ndugu Ezekiel Assecheck ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Ustawi wa Jamii amesisitiza umuhimu wa jamii na wadau kuendelea kushirikiana katika kulinda haki za mtoto wa kike, akibainisha kuwa uwekezaji katika elimu ya afya ni msingi muhimu wa kumjengea msichana maisha salama na yenye tija.


Kwa upande wake, Carol McDonald kutoka taasisi ya CHaRA ameeleza kuwa taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na halmashauri ya Wilaya ya Mbulu katika utekelezaji wa programu zinazolenga kuzuia ukatili wa kijinsia na kuboresha afya na ustawi wa watoto na vijana, hususan wasichana.


Halmashauri inaendelea kupongeza mchango wa wadau wote wanaoshirikiana katika juhudi za kuinua elimu, afya na ustawi wa jamii, na inaahidi kuendeleza ushirikiano huo ili kuhakikisha mazingira salama na rafiki kwa watoto, hasa mtoto wa kike.




Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI October 20, 2025
  • TANGAZO LA USAFI JUMAMOSI YA MWISHO YA MWEZI November 28, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA (JKT) KWA HIARI January 27, 2026
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • USHIRIKIANO WA KITENGO CHA USTAWI WA JAMII NA TAASISI YA CHaRA WAWEZESHA WANAFUNZI WA KIKE DONGOBESH SEKONDARI KUPITIA ELIMU YA AFYA, KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA NA UGAWAJI WA TAULO ZA KIKE

    February 09, 2026
  • WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WANUFAIKA NA MIKOPO YA ASILIMIA 10 MBULU DC

    January 19, 2026
  • WANANCHI WAASWA KUENDELEA KUCHUKUA TAHADHARI YA UGONJWA WA UKIMWI

    December 01, 2025
  • MADIWANI MBULU DC WAASWA KUZINGATIA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

    December 03, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

DC SEMINDU AAGIZA WATENDAJI KUHAKIKISHA WANASIMAMIA UTOAJI WA LISHE KILA KIJIJI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.