• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Dinamu
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

WANANCHI MANYARA WAHIMIZWA LISHE BORA KUKABILIANA NA UDUMAVU

Kurushwa hewani: June 21st, 2024


MBULU-MANYARA 

Jamii mkoani Manyara imetakiwa kuzingatia makundi muhimu ya vyakula kwa watoto wa umri chini ya miaka mitano na wanawake wajawazito ili kukabiliana na hali ya udumavu na uzito mdogo kwa watoto inayokabili mkoa huo ambao takwimu zinaonesha asilimia 32 ya watoto imedumaa.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa mkoa wa Manyara QUEEN SENDIGA katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na mkuu wa wilaya ya Mbulu VERONICA KESSY katika maadhimisho ya siku ya Lishe mkoa wa Manyara iliyofanyika wilayani MBULU.

Kwa mujibu wa Utafiti wa hali ya lishe nchini uliofanywa na Tanzania Demographic Survey mwaka 2022,  asilimia 32 ya watoto wenye umri wa mwaka 0 hadi miezi 59 mkoani Manyara wamedumaa, asilimia 19.6 wana uzito mdogo na asilimia 4.7 wana ukondefu.

Hiyo ndiyo iliyosukuma wizara ya afya kufanyia maadhimisho hayo mkoani MANYARA kushirikiana na shirika la TAHA wakitumia wataalamu wa lishe kutoa elimu ya lishe pamoja na kuhimiza kilimo cha mbogamboga na wanyama wadogo kwa ajili ya matumizi kaya ili kukabiliana na udumavu.

Mkuu wa wilaya ya Mbulu VERONICA KESSY licha ya kuhimiza Wananchi kilimo cha mbogamboga pamoja na ufugaji wa wanyama wadogo kwa ajili ya matumizi ya chakula cha kaya pia amekemea tabia ya unywaji pombe haramu ya gongo hasa kina mama kuwanyesha watoto pombe kwa lengo la kuwafanya wapate usingizi ili wafanye shughuli zao kwamba kufanya hivyo ni hatari kwa afya ya watoto kwani wanatengeneza usugu wa pombe na kuwadumaza watoto.

Kaimu afisa mtendaji mkuu wa TAHA ANTONY MANGA ametoa wito kwa jamii mkoani humo kujenga mazoea ya  kula makundi yote muhimu ya vyakula ili kukabiliana na hali ya udumavu, uzito mdogo na ukondefu.

Pia ameahidi kuwa TAHA itashirikiana na wilaya hiyo kuanzisha kilimo cha zao la Parachichi kutokana na hali ya hewa ya wilaya hiyo kuruhusu zao hilo kustawi na kwamba hiyo itachangia kuongeza kipato cha wanafamilia na mkoa huo.

"Tunashukuru wafadhili wetu shirika la kimataifa la maendeleo la serikali ya SWEDEN kutuwezesha kuandaa siku hii na kugusa maisha ya jamii kupitia elimu ya lishe"

Kijiji cha LAGANGESH kilichopo katika kata ya YAEDA HHAMPA yalikofanyika maadhimisho hayo ni moja ya eneo ambalo hali ya lishe ni duni zaidi.

Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu, PETRO TARMO ameshukuru kwa fursa hiyo ya kupewa elimu katika maadhimisho hayo yaliyoambatana na maonesho ya makundi mbalimbali ya vyakula pamoja na upimaji bure wa afya na ushauri kuhusu lishe kutoka kwa wataalamu mbalimbali wa TAHA, wizara, mkoa na wilaya.

Naye Diwani wa viti maalum, NURUANA KIPAPAI amesema atatumia elimu aliyopata katika maadhimisho hayo kwenda kuelimisha jamii kupitia mikutano mbalimbali.

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya siku ya lishe mwaka huu ni "Lishe bora kwa afya njema na ustawi wa Taifa"

 




Matangazo

  • Tangazo la fursa za mafunzo ya ufundi stadi awamu ya saba February 01, 2025
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • JINSI YA KUTOA/KUTUMA MALALAMIKO KWA NJIA YA MTANDO HALMSHAURI YA WILAYA YA MBULU. March 23, 2019
  • KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU 2021 June 10, 2021
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • MBULU DC YATOA SADAKA KITUO CHA AFYA DONGOBESH.

    January 30, 2025
  • MBULU DC YAKWAMUA VIKUNDI VYA VIJANA KIUCHUMI

    February 13, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 38.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZA WANAFUNZI WARIPOTI SHULENI

    January 31, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

MBULU DC KUKUSANYA ZAIDI YA MIL.90 KATIKA MSIMU MPYA WA UVUVI KUTOKA BWAWA LA BONDELA YAEDA CHINI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.