• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Dinamu
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

WAZIRI JAFO AKABIDHI BILIONI 4 KWA WANUFAIKA WA HEWA UKAA MANYARA.

Kurushwa hewani: November 14th, 2023

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Dokta Suleyman Jafo amewataka wamiliki wa biashara ya Carbon Tanzania wafanye mgawanyo wa hela sambamba na kanuni ya nne ya Carbon kipengele cha C, ya uwazi katika biashara ya Carbon na ijulikane tani ngapi zimeenda kuuzwa na kwa kiasi gani.

Hayo yalisemwa na Waziri Jafo katika kikao cha kukabidhi cheki ya bilioni 4, 740, 7000.00 ikiwa ni faida ya biashara ya hewa ukaa inayofanyika kwa uhifadhi wa misitu na mazingira chini ya usimamizi wa Taasisi ya Carbon Tanzania kwa wilaya nufaika za miradi huo ambazo ni Wilaya ya Mbulu na Wilaya ya Kiteto, kilichofanyika katika ukumbi wa White Rose Babati, Mkoani Manyara Novemba 14, 2023.

“Tulitoa maelekezo ya kampuni zote zinazoshiriki biashara ya Carbon, kwanza zifanye usajili/registration, na mpaka leo hii ninavyozungumza Zaidi ya makampuni 33 yameshajisajili katika biashara ya Carbon nchini Tanzania, na katika makampuni hayo, makampuni 12 tumeshayapa no objection letter. Na kampuni ya Carbon Tanzania tumeshawapa endorsement letter, hongereni sana.” Alisema Waziri Jafo.

Aidha Waziri Jafo alisema kuwa serikali inataka watu wabadilike,na kuongeza katika biashara hii ya Carbon wanatarajia kwanza ajira nyingi zipatikane katika maeneo ya wakazi wa mradi na itakuwa ni fursa ya ajira.Lakini pili pato litakuja kwenye Serikali itakayokuwa inahudumia wananchi kwa rasilimali zake zilizokuwa nazo.

Waziri Jafo amewapongeza na kuwasifu Carbon Tanzania kwa kazi kubwa wanayoendelea kuifanya,lakini pia amewaomba maarifa mengine ya uwazi na utunzaji wa kanuni waifanyie kazi katika toleo lijalo la mgao.Pia amewaomba wananchi watunze misitu yao kwa sababu misitu ni mali na agenda ya kutunza mazingira ni agenda ya kudumu kwetu sote.

Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga amesema kuwa anawashukuru sana watu wa Carbon Tanzania kwa kazi kubwa wanayoifanya na kuona umuhimu wa kufanya shughuli hii leo na ni kwa mara ya kwanza tumekusanya kusanyiko kama hili la wanufaika na kuweza kuwapatia fedha hizi wao wenyewe moja kwa moja mbele yako wewe Waziri mwenye dhamana.

Kwa upande mwengine RC queen amesema kuwa wamepata faida nyingi kupitia mradi huo ikiwemo utunzaji wa mazingira,utekelezaji wa mpango wa matumizi bora ya ardhi.Faida ambayo tunapata ni kubwa sana na kwa wenzetu kule Mbulu wameendelea kupata hii faida katika vijiji vitano,na mradi umeendelea kutoa matokeo mazuri.Eneo ambalo limetengwa kule ni Zaidi ya hekta laki moja na kumi ambazo zinaendelea kufanyiwa kazi.Na wanufaika wa mradi huu ni Zaidi ya watu elfu sitini na nne katika mradi huu ambao wameendelea kupata faida ya kuboreshewa huduma za kijamii.

Naye Mkuuu wa Wilaya ya Mbulu Kheri James amesema kuwa kwa mara ya kwanza tunaanza kuwaona watoto wanaotoka katika jamii za wafugaji wanasoma kwenye shule nzuri,wanapata elimu bora na kwa viwango wanavyovitaka,na wengine wapo hadi vyuo vikuu kupitia program hii.Lakini pia inawasaidia kuwa sawa kwenye soko la ushindani wa ajira, lakini unyonge huo umeondoka.

Aliendelea kusema kuwa pamoja na faida hizo za kimazingira, mpango huu wa uvunaji wa hewa ya ukaa umechochea matumizi bora ya ardhi ndani ya Wilaya.Na mpango wa ardhi unapoimarika unatusaidia kupunguza migogoro ya ardhi.Aidha biashara ya hewa ukaa katika Wilaya ya Mbulu ipo katika maeneo ya Yaeda chini, Mongo wa mono, Domanga, Eshkesh na Endanyawish.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Fedha wa Carbon Tanzania, Alphael Jackson amesema kuwa mradi wa hewa ya ukaa katika bonde la Yaeda ulianza mwaka 2013 ikiwa chini ya Halmashauri ya Mbulu,ikihusisha jamii za Wahadzabe, mongo wa mono,Domanga na  Yaeda chini.Na tulianza na vijiji viwili lakini tulilenga Zaidi upande wa Wahadzabe.

Aliendelea kusema kuwa mradi unahusisha misitu iliyopo ndani ya vijiji kwa kuzingatia mpango wa matumizi bora ya ardhi,yenye ukubwa wa hekta laki moja na kumi mia tano ishirini na sita na yenye jumla ya wakazi elfu sitini na nne wanaonufaika na mradi huu wa hewa ukaa.

“Mradi una lengo la kuhifadhi mazingira,sisi tunaangalia misitu Zaidi na ni misitu ya asili,kutunza vyanzo vya maji,mradi umelenga kuboresha huduma kwa  jamii katika kuhifadhi na kunufaika moja kwa moja na faida za uhifadhi.”Alisema Alphael.

Matangazo

  • Tangazo la fursa za mafunzo ya ufundi stadi awamu ya saba February 01, 2025
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • JINSI YA KUTOA/KUTUMA MALALAMIKO KWA NJIA YA MTANDO HALMSHAURI YA WILAYA YA MBULU. March 23, 2019
  • KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU 2021 June 10, 2021
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • MBULU DC YATOA SADAKA KITUO CHA AFYA DONGOBESH.

    January 30, 2025
  • MBULU DC YAKWAMUA VIKUNDI VYA VIJANA KIUCHUMI

    February 13, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 38.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZA WANAFUNZI WARIPOTI SHULENI

    January 31, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

MBULU DC KUKUSANYA ZAIDI YA MIL.90 KATIKA MSIMU MPYA WA UVUVI KUTOKA BWAWA LA BONDELA YAEDA CHINI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.