• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Dinamu
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

Dk.Ndugulile ahidi kutoa Bilioni Moja kuanza Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.

Kurushwa hewani: November 4th, 2018


Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile akikagua stoo kuu ya kuhifadhi dawa katika hospitali ya Rufaa ya Haydom


Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile  amefanya ziara ya kikazi Mkoani Manyara na kutembelea halmashauri ya Wilaya ya Mbulu ili kujionea shughuli mbalimbali  katika  Hospitali ya Rufaa ya Haydom na Kituo cha Afya cha Dongobesh, akiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Haydom  aliweza kupokea taarifa ya hospitali na kisha kutembelea sehemu mbalimbali ndani ya hospitali kujionea huduma zitolewazo.

Mganga Mkuu wa Hospitali Dokta Emanuel Nuwasi akisoma taarifa ya utendaji ya hospitali ya rufaa ya Haydom


Akisoma taarifa ya Hospitali ya Rufaa ya Haydom,Mganga Mkuu wa Hospitali Dokta Emanuel Nuwasi aliweza kueleza changamoto mbalimbali zinawazowakabili ikiwa ni pamoja na changamoto ya ufinyu wa bajeti,changamoto ya bajeti ndogo ya dawa tofauti na mahitaji, vitendanishi tiba kutoka bohari ya dawa(MSD), Kuharibika kwa Mashine ya CT SCAN, kukatwa kodi kwa Call Allowance,changamoto kwa Watumishi wanaolipwa kwa Ruzuku( Salary Grant),kucheleweshwa kusainiwa kwa makubaliano maalum juu ya utoaji huduma (MOU),kuondokewa kwa Watumishi kutokana na mazingira

Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile akikagua chumba cha kuhifadhi damu salama.


Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile akifurahi mara baada yakukuta taarifa za wagonjwa zikiingizwa katika mfumo.

Mara baada ya kupokea taarifa ya Hospitali Dokta Faustine alihaidi kwenda kushughulikia changamoto hizo zinazowakabili kutokana na hospitali hiyo kuwa kwenye mchakato wa kupandishwa hadhi kuwa hospitali ya Rufaa ya Kanda,aidha Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine alitoa ushauri kwa uongozi kuweza kutekeleza maagizo waliyopewa na kamati iliyoundwa na Waziri Mkuu ili hospitali hiyo iweze kupandishwa hadhi mapema.


Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile akiongea na baadhi ya wananchi walikuja kutembelea wagonjwa katika wodi la wazazi


Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile akiwa katika wodi la wanaume akikagua taarifa za mgonjwa mmojawapo 

Sambamba na maagizo hayo Dkt. Faustine ameendelea kuhimiza kusimikwa kwa Mfumo wa Afya (GoTHOMIS) ili kuweka kumbukumbu sahihi za Wagonjwa,Madawa yanayotoka na na kuingia pamoja na kudhibiti Mapato yanayokusanywa ,pia alipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu kwa sasa kutokuwa na kituo cha Afya/Zahanati yoyote yenye hadhi ya nyota 0 na hatimaye kuweza kukabidhi cheti cha hadhi ya nyota 2 kwa zahanati ya Labay.


Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile akipitia kwa makini taarifa ilikuwa inawasilishwa.

Watumishi wa Hospitali ya rufaa ya Haydom wakiwa ukumbini wakimsikiliza  Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile 

Akiongea na wananchi kwenye mkutano wa hadhara kata ya dongobesh, Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile amehaidi kuleta fedha kiasi cha Bilioni moja mwisho wa mwezi huu,hii ni kutokana na Serikali imekwisha leta kiasi cha shilingi Milioni 500 ambazo ni kwa ajili ya Ujenzi wa hospitali ya Wilaya kwa kutumia nguvu ya wananchi( force account), hivyo kuagiza fedha hizo zitakapoingia ujenzi huo uanze mara moja.

Wananchi wa kata ya Dongobesh wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika viwanja vya kata ili kumsikiliza Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile


Waheshimiwa Madiwani wa Viti Maalum kata ya Dongobesh kwa tiketi ya CCM, Mhe. kipapai na Mhe. Esther wakikabidhi zawadi ya Shuka( mgoroli),Kitenge na Vitunguu Swaumu Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile

Akihitimisha ziara yake Wilayani Mbulu,Dokta Faustine amehimiza kuanza mkakati mapema wa kutoa elimu juu ya lishe bora na kuandaa mpango mkakati wa matumizi ya vyoo bora.

Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile akipata maelezo zaidi juu ya ujenzi wa chumba cha kuhifadhi Maiti kutoka kwa Mhandisi wa Halmashauri mwenye shati jeupe Mhandisi Bundala.

Matangazo

  • Tangazo la fursa za mafunzo ya ufundi stadi awamu ya saba February 01, 2025
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • JINSI YA KUTOA/KUTUMA MALALAMIKO KWA NJIA YA MTANDO HALMSHAURI YA WILAYA YA MBULU. March 23, 2019
  • KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU 2021 June 10, 2021
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • MBULU DC YATOA SADAKA KITUO CHA AFYA DONGOBESH.

    January 30, 2025
  • MBULU DC YAKWAMUA VIKUNDI VYA VIJANA KIUCHUMI

    February 13, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 38.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZA WANAFUNZI WARIPOTI SHULENI

    January 31, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

MBULU DC KUKUSANYA ZAIDI YA MIL.90 KATIKA MSIMU MPYA WA UVUVI KUTOKA BWAWA LA BONDELA YAEDA CHINI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.