Na, Ruth Kyelula.
Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Jackline David, ametoa wito kwa jamii kuhimizana wao kwa wao juu ya masuala ya lishe bora na kuzingatia ulaji unaofaa ili kuweza kukabiliana na tatizo la utapiamlo mkali katika jamii.
Afisa Lishe wa Wilaya, Jackline David akielezea shughuli za lishe zilizofanyika kwa robo ya tatu.
Hayo aliyasema wakati wa kikao cha Tathimini ya hali ya Lishe cha robo ya tatu ambacho kilikaa na watendaji wa Kata 18, Mkuu wa Wilaya, DAS na wataalamu, Katika ukumbi wa Halmashauri Mei 08, 2025.
Kwa upande mwingine amewataka wanaume washiriki katika mikutano ya siku ya afya na lishe ya vijiji ili elimu ya lishe, malezi na makuzi ya watoto iweze pia kuwafikia wao moja kwa moja.
Baadhi ya Wataalamu wa Halmashauri wakifuatilia wasilisho la utekelezaji wa shughuli za Lishe kwa robo ya tatu.
Aidha Afisa Lishe alisema baadhi ya shughuli walizozifanya kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2025 ni utoaji wa matone ya vitamin A kwa watoto 35400, uchunguzi wa hali ya lishe kwa watoto 1254 waliolazwa wodini, kutoa mafunzo kwa wahudumu wa Afya ngazi ya jamii 35 (CHW) na wamefanya ziara shirikishi katika shule za msingi 10 na sekondari 10 zilizoanzishwa bustani za mboga mboga.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Michael Semindu alisema kuwa, watendaji wote wanatakiwa wawe wanamtumia taarifa za siku na kila mwezi ya matukio yote yanayoendelea katika kata zao bila kusahau kutembelea miradi yote iliyopo maeneo yao na kuifanyia ukaguzi wa mara kwa mara ili kuepuka hasara zinazoweza kujitokeza.
Mwisho Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Abubakar Kuuli alimshukuru Mkuu wa Wilaya kwa maelekeo aliyoyatoa na kuongeza kuwa yeye ni muumini wa masuala mazima ya Lishe, yote aliyoyasema wataenda kuyatekeleza.
Watendaji wa Kata 18 wakifuatilia wasilisho la Lishe.
Mbulu district Coucil
Anuani: P.O.BOX 74
Simu ya mezani: +255743583078
Simu: +255716992222
Barua pepe: md@mbuludc.go.tz
Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.