• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Dinamu
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

Kamati ya Siasa Wilaya ya Mbulu Yasifu Ubora wa Miradi ya Maendeleo Kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Tarehe 28.09.2021

Kurushwa hewani: September 28th, 2021


Kamati ya Siasa Wilaya ya Mbulu Ikiwa Katika Mtambo wa Mradi wa Maji Mbulu Kulia ni Meneja wa Wakala wa Maji Mjini na Vijijini Akifafanua Jambo Katika Mradi Huo.


Kamati ya Siasa Wilaya ya Mbulu, Ikiwa Katika  Mradi wa Ujenzi wa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Kata ya Dongobesh.


Kamati ya Siasa Wilaya ya Mbulu, Ikiwa Katika  Mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Kata ya Dongobesh.


Kamati ya Siasa Wilaya ya Mbulu, Ikiwa Katika  Mradi wa Barabara ya Lami Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Kata ya Dongobesh.

Aliyesimama ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mbulu Mh. Mhandisi, Melkiadi Nari Akizungumza Katika Kikao cha Majumuisho Leo Tarehe 28.09.2021.

Aliyesimama ni Mh.Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Sezaria V. Makota Akizungumza Katika Kikao Hicho cha Majumuisho Leo Tarehe 28.09.2021.







~~~~~~~~~~~     HABARI KAMILI     ~~~~~~~~~~~



Haya yamejiri leo baada ya kamati husika kuwa na ziara ya siku moja ya kukagua miradi ya maendeleo kwa wananchi inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri yawilaya ya Mbulu. Kamati hii inautaratibu wa kukagua miradi ya maendeleo ili kujiridhisha kuhusiana na mapokezi ya fedha za serikali, mapato ya ndani, na utekelezaji kwa vitendo kwa hizi fedha kwenye miradi husika ili kupunguza kero za wananchi na kuleta maendeleo.


Kimsingi miradi iliyotembelewa ni ujenzi wa barabara za lami makao makuu ya wilaya ya Mbulu Kata ya Dongobesh kiasi cha kilometa 10 katika mitaa ya Kata ya Dongobesh ambayo inasimamiwa na ofisi ya Wakala wa barabara mijini na vijijini (TARURA), miradi ya maji inayosimamiwa na Wakala wa Maji Mjini na Vijijini, mradi wa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, mradi wa Hospitali ya Wilaya iliyoko Kata ya Dongobesh na mwisho ni ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa na ofisi 1 Shule ya Sekondari Bishop Hando ambao unasimamiwa na Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu chini ya Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji.


Katika miradi yote waliyopita kamati imeridhishwa na viwango vya hali ya juu vya ubora wa miradi na thamani ya fedha zilizotumika katika miradi yote hii kwa kila mmoja wao na kuwapongeza wataalamu kuanzia Wahandisi, Mameneja na Menejimenti kwa ujumla wao hadi kufanikisha katika hatua inayoonekana kwa sasa.


Hata hivyo Mh.Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Sezaria V. Makota ambaye ndiyo mwenyeji wao kwa Wilaya ya Mbulu ameahidi kwamba ataendelea kuwasimamia wataalamu wote ili kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi na kwa wakati kiasi kwamba siku zote tuwe na miradi mizuri ya kiwango cha juu kwani miradi inapokuwa ni mizuri thamani ya fedha inaonekana hivyo wananchi kuwapunguzia kero kama mlivyoona kero ya maji imepungua, elimu kwa unjenzi wa vyumba vya madarasa na waaalimu kupata ofisi, kuwepo kwa barabara kunaongeza mvuto wa wananchi kufanya biashara na kila pahali pa mji sasa panaonekana na panapendeza.


Mh.Mkuu wa Wilaya ya Mbulu anaishukuru sana serikali kwa kuleta fedha hizi katika Wilaya ya Mbulu anaomba kuendelea kuongeza katika miradi mingine kwa hawa wananchi kwani fedha zote zitatumika kwa kufuata kanuni na taratibu za kisheria.

Matangazo

  • Tangazo la fursa za mafunzo ya ufundi stadi awamu ya saba February 01, 2025
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • JINSI YA KUTOA/KUTUMA MALALAMIKO KWA NJIA YA MTANDO HALMSHAURI YA WILAYA YA MBULU. March 23, 2019
  • KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU 2021 June 10, 2021
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • MBULU DC YATOA SADAKA KITUO CHA AFYA DONGOBESH.

    January 30, 2025
  • MBULU DC YAKWAMUA VIKUNDI VYA VIJANA KIUCHUMI

    February 13, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 38.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZA WANAFUNZI WARIPOTI SHULENI

    January 31, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

MBULU DC KUKUSANYA ZAIDI YA MIL.90 KATIKA MSIMU MPYA WA UVUVI KUTOKA BWAWA LA BONDELA YAEDA CHINI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.