• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Dinamu
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

KURUGENZI CUP ’18 YATIMUA VUMBI MBULU KWA KAMOGA

Kurushwa hewani: May 13th, 2018

Mji mdogo wa Haydom wa Wilayani Mbulu Mkoani Manyara na viunga vyake kwa muda wa wiki hii nzima utakumbwa na burudani kubwa kupitia tamasha la ujasiriamali na michuano ya Kurugenzi Cup ’18 iliyoandaliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Hudson Kamoga. 

Pamoja na mada za ujasiriamali kutolewa pia michuano ya soka itakayoshirikisha timu 10 itatimua vumbi kwenye viwanja vya Haydom na kufikia tamati jumapili ya Mei 20. 

Kamoga akizungumza wakati wa ufunguzi wa tamasha na michuano hiyo alisema lengo la kuandaa ni kusisitiza uzalendo wa vijana na jamii kwa ujumla kuipenda nchi yao. 

Kamoga alisema anatarajia vijana watajinyanyua kiuchumi kwa kufanya kazi kupitia kauli mbiu ya tamasha hilo isemayo wakati wa kuwa mzalendo na kujenga nchi yetu, uvivu ni sumu ya maendeleo. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Kamoga akikagua timu ya Kidarafa FC kwenye ufunguzi wa michuano ya Kurugenzi CUP ’18 inayoshirikisha timu 10 na kufanyika kwenye viwanja vya Haydom ambapo pia kutakuwa na matamasha mbalimbali ikiwemo semina ya ujasiriamali.

Alisema kwa muda wa wiki moja itakayofanyika tamasha hilo kutakuwa na mada mbalimbali za ujasiriamali zitakazotolewa na magwiji mbalimbali waliobobea kwenye uchumi. 

“Wilaya ya Mbulu ina fursa nyingi na vichocheo vya kiuchumi hivyo tutawatumia watu maarufu akiwemo mchambuzi wa soka Shafi Dauda ambaye atakuja hapa Haydom,” alisema Kamoga. 

Alisema wanatarajia kuibua vipaji vipya tofauti kwenye soka na riadha ili vijana wafuate nyayo za mwanariadha maarufu wa zamani John Stephen aliyeacha historia kwenye michuano ya dunia. 

“Kwa muda wa wiki hii nzima kutakuwa na shamrashamra kwenye mji mdogo wa Haydom na wilaya ya Mbulu kwa ujumla ambapo wageni mbalimbali watakuja kwenye tamasha na mashindano haya yatakayohitimishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo siku ya jumapili ijayo,” alisema Kamoga.

 Hudson Kamoga akitakiana kheri na mwamuzi  kwenye michuano ya Kurugenzi CUP ’18 itakayoshirikisha timu 10 na kufanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Haydom.


 Baadhi ya timu shiriki toka dongonesh na kidarafa zikiwa zimebeba ujumbe wa maadhimisho ya wiki ya ujasiliamali wakati wa uzinduzi wa michuano ya Kurugenzi CUP ’18 kwa kufunga bao,michuano hiyo itashirikisha timu 10 na kufanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Haydom ambapo pia kutakuwa na matamasha mbalimbali ikiwemo semina ya ujasiriamali.

Aidha Katibu wa chama cha soka cha wilaya ya Mbulu (MDFA) Joseph Nicodemus alitaja timu zitakazoshiriki michuano hiyo ni Dongobesh FC, Young Boys, Airport SC, Qadesh SC, Mlimani City Lambo FC, Stand United, Makurusa SC, Rema 1,000 na Kidarafa FC ya wilaya jirani ya Mkalama Mkoani Singida. 

Nicodemus alisema michuano hiyo itakayofanyika kwa muda wa wiki moja itatumia mtindo wa mtoano na siyo ligi, hivyo timu ikifungwa inatolewa mashindanoni. 

Kwenye ufunguzi wa michuano hiyo, timu ya Dongobesh FC iliifunga timu ya Kidarafa FC ya wilayani Mkalama mkoani Singida mabao 2-1 na mchezo mwingine uliofanyika siku iliyofuata timu ya Stend United (Chama la wana) ya Mji mdogo wa Haydom iliifunga Mlimani City ya Ng’wandakw bao 1-0 na mchezo wa kesho jumatano utazikutanisha timu ya Young Boys na Airport SC. 


Mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Mbulu ndugu Hudson Kamoga akiwa picha ya pamoja na viongozi wa michezo Wilaya, Viongozi wa timu shiriki na wadau wa michezo Wilayani.

Matangazo

  • Tangazo la fursa za mafunzo ya ufundi stadi awamu ya saba February 01, 2025
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • JINSI YA KUTOA/KUTUMA MALALAMIKO KWA NJIA YA MTANDO HALMSHAURI YA WILAYA YA MBULU. March 23, 2019
  • KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU 2021 June 10, 2021
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • MBULU DC YATOA SADAKA KITUO CHA AFYA DONGOBESH.

    January 30, 2025
  • MBULU DC YAKWAMUA VIKUNDI VYA VIJANA KIUCHUMI

    February 13, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 38.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZA WANAFUNZI WARIPOTI SHULENI

    January 31, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

MBULU DC KUKUSANYA ZAIDI YA MIL.90 KATIKA MSIMU MPYA WA UVUVI KUTOKA BWAWA LA BONDELA YAEDA CHINI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.