Na Magreth Mbawala, Mbulu DC.
Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu leo tarehe 03/12/2025 wamekula kiapo cha maadili ya uongozi wa umma pamoja na mafunzo kuhusu ujazaji wa tamko la rasilimali na madeni ya viongozi.
Kiapo hiko kimeongozwa na Adam Kuhanda Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais Sekretarieti ya maadili ya viongozi wa umma kanda ya Kaskazini ambapo amewaasa madiwani kuweka wazi mali zote wanazozimiliki bila kuficha chochote kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria na watawajibishwa.
Pia aliwasisitiza kuwa taarifa hizo zinajazwa ndani ya siku 30 mara baada ya kuchaguliwa kwao.Hivyo wafanye hima kujaza kuepuka usumbufu.
Aidha Bwana Kuhanda aliwakumbusha madiwani kuanza kuishi maadili ya kiuongozi ikiwa ni pamoja na mavazi wanayovaa,kuongea,kula na kuishi na watu kwenye jamii .
Naye Afisa wa TAKUKURU wa Wilaya ya Mbulu Lawrence Mlaponi, aliwataka Madiwani kuepuka vitendo vya rushwa kwa kuacha kutoa na kupokea rushwa.Pia aliwataka kuacha kupokea zawadi kutoka kwa wanaowaongoza kwani ndio chanzo cha kutokutenda haki.
Sambamba na hilo aliwasihi kwenda kusimamia vema miradi ya maendeleo kwenye kata zao na kuacha kuangalia maslahi yao binafsi kwenye miradi ya umma ikiwemo kutaka asilimia kumi.
Mwisho Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mhe. Yeconia Maleyecky aliwashukuru watoa mada kwa Elimu nzuri waliyowapatia.
Mbulu district Coucil
Anuani: P.O.BOX 74
Simu ya mezani: +255743583078
Simu: +255716992222
Barua pepe: md@mbuludc.go.tz
Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.