Na, Ruth Kyelula, Mbulu DC,
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Joseph Mandoo, amewapongeza waheshimiwa Madiwani kwa usimamizi mzuri wa kazi za miradi katika kata zao, kwa kuchangisha, kuleta changamoto na vipaumbele vya wananchi kupitia kamati ya maendeleo ya kata.
Mkuu wa shule ya sekondari Dr. Olsen, Veronica Mmasi,akikabidhiwa cheti cha pongezi na Mhe.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Joseph Mandoo, kwenye baraza la madiwani
Hayo aliyasema Mhe.Mandoo wakati akifungua kikao cha baraza la Madiwani la robo ya tatu 2024/2025, katika ukumbi wa Halmashauri, Aprili 29,2025.
Aidha Mhe.Mandoo amempongeza Mkuu wa shule ya sekondari Dr. Olsen, Veronica Mmasi, kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari Basonyagwe, inayojengwa kwa gharama ya Tsh. 584,280,029. -00, katika Kata ya Haydom.
“Na sio tu mradi wa Basonyagwe, amekuwa mstari wa mbele pale tu, tunapopeleka fedha kwenye kata ya Haydom, hasa miradi ya Elimu upande wa sekondari, amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa .Tunahitaji wakuu wa shule wa aina hii kwenye Halmashauri yetu.” Alisema Mandoo.
Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu wakifuatilia kikao cha baraza
Kwa upande mwingine Mhe. Mwenyekiti, alisema tunazo changamoto mbalimbali kwenye miradi yetu,na amewaomba waheshimiwa Madiwani kwa muda uliobaki, waendelee kutatua zile changamoto na waboreshe usimamizi wa miradi.
Kwa upande wake Katibu wa Baraza na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Abubakar Kuuli, aliwapongeza Madiwani wote kwa kazi nzuri ambazo wamekuwa wakizifanya katika Kata zao, akitolea mfano Kata ya Haydom ambapo kuna ujenzi wa shule mpya ya sekondari Basonyagwe, shule ambayo imeingia kwenye historia ya Halmashauri na kuongeza kuwa nguvu ya ufuatiliaji ilikuwa ndogo sana, lakini mradi umekamilika kwa viwango na chenji zimebaki.
“Pale Labay tuna mradi wa barabara, na wale wenzetu walikua wanahitaji maeneo kwa ajili ya kupata kokoto, Mhe. Diwani pale ametusaidia. Hii ni kwa mifano tu lakini kata nyingi mambo yamekwenda vizuri. Halikadhalika kwa maafisa Tarafa na wakuu wa Idara, pia niwapongeze kwa kazi nzuri mnazoendelea kuzifanya. Mfano mzuri maafisa Elimu walipongezwa kwenye mkutano wetu wa Ilani, kupongezwa kwa maafisa Elimu maana yake tumepongezwa CMT yote.” Alisema Kuuli.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Abubakar Kuuli, akizungumza wakati wa baraza la madiwani.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Michael Semindu, alisema kuwa Mhe.Rais ameshatimiza wajibu wake, ameleta barabara, hela za maji,za elimu na sekta nyingine zote, jukumu letu sisi kwenye ngazi ya Wilaya,Kata,Vijiji na Tarafa, ni kuhakikisha huduma bora zinatolewa kwa wananchi wetu na mtumie lugha rahisi ambayo watu wataielewa.
Mwisho Mbunge wa Mbulu Vijijini, mhe. Flatei Massay alisema kuwa anamshukuru Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwafaa wana Mbulu na Watanzania kwa ujumla kwa kuwajengea jengo la Halmashauri lenye thamani ya Zaidi ya Bilioni 5, hospitali kubwa ya Wilaya yenye thamani ya tsh. 3,628,000,000/=
Mbulu district Coucil
Anuani: P.O.BOX 74
Simu ya mezani: +255743583078
Simu: +255716992222
Barua pepe: md@mbuludc.go.tz
Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.