• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Dinamu
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

MBULU DC KINARA UKUSANYAJI WA MAPATO- MANYARA.

Kurushwa hewani: January 30th, 2024

Na, Ruth Kyelula – Afisa Habari Mbulu DC. 

Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Kheri James ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu kwa kuwa kinara wa ukusanyaji wa mapato katika mkoa wa Manyara.

Hayo aliyasema wakati akitoa hotuba yake katika kikao cha robo ya pili 2023/24 cha baraza la Madiwani, kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri na kuhudhuriwa na Madiwani, timu ya wataalam pamoja na kamati ya usalama, Januari 30,2024.

“Niwapongezeni sana Halmashauri kwa kazi kubwa na nzuri ambayo mnaifanya, ninafurahishwa sana na zoezi la mapato, kwenye mapato kwa kweli hakuna wakufanana nae, hakuna mfano kabisaa hapa ndani ya Wilaya wala Mkoa mzima. Sisi bado tumeshikilia kinara cha mkoa wa Manyara kwenye ukusanyaji wa mapato. Na mimi nataka niwaambieni kwa spidi hii mnanisababisha nitembee kifua mbele kwamba mwaka huu pia Halmashauri ya Wilaya hii itaongoza katika kukusanya mapato katika mkoa wa Manyara.” Alisema Mkuu wa Wilaya Kheri James.

Kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya pili 2023/24

DC Kheri, ameendelea kushauri kutokana na mvua zinazoendelea wananchi kuweka akiba ya chakula ili hata endapo hawatavuna wawe na akiba ya chakula mvua zikiondoka.Lakini pia amewaasa wananchi kuepuka safari zisizo na ulazima na ikiwezekana kuziepuka kabisa.

Kwa upande mwingine Mbunge wa Mbulu vijijini, Flatei Massay amesema kuwa kutokana na changamoto ya mvua barabara nyingi kuharibika na mawasiliano mengi kukatika,pamoja na madaraja kuchukuliwa,ameiagiza TARURA kufanya utafiti wa haraka ili aombe fedha kutoka serikali kuu kwa sababu katika kata zote kumi na nane hakuna iliyo na unafuu.


Mbunge wa Mbulu vijijini Mhe.Flatei Massay akitoa hotuba yake katika Baraza la Madiwani Januari 30,2024. 

“Niwapeni pole sana wananchi ambao wamepoteza ndugu zao kutokana na mafuriko yaliyotokea  na maeneo mengi,poleni sana kwa kupoteza  familia mana najua kata nyingi watu wengi wamechukuliwa na maji, Mungu aziweke roho za marehemu wote mahali pema peponi.” Alisema Mhe. Flatei.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri, Mheshimiwa Joseph Mandoo, alimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, pamoja na timu ya Wataalamu kwa jinsi ambavyo wameendelea kukusanya mapato ya ndani, ambayo kwayo Halmashauri yetu imeendelea kushika nafasi katika mkoa wa Manyara.

Baadhi ya Madiwani wakifatilia ajenda mbalimbali za kikao.

“Hadi Desemba Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu tumekusanya mapato kwa asilimia 83%, ni jambo la kujivunia. Lakini bado hatutabweteka kwa sababu tunatakiwa tuone fursa mbalimbali zinazowezesha Halmashauri kuongeza mapato ya ndani, lakini kuwezesha kuona fursa fichwa ambazo sisi kama wajumbe wa baraza na wataalamu wetu hatukuweza kuona katika mapato yetu ya ndani.” Alisema Mhe. Mandoo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Abubakar Kuuli alisema kuwa kwa upande wa Halmashauri tunaendelea salama na tunaendelea na makusanyo pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Ijapokuwa hali ya hewa ya mvua si rafiki katika shughuli zetu tunazoendelea nazo za miradi.

Matangazo

  • Tangazo la fursa za mafunzo ya ufundi stadi awamu ya saba February 01, 2025
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • JINSI YA KUTOA/KUTUMA MALALAMIKO KWA NJIA YA MTANDO HALMSHAURI YA WILAYA YA MBULU. March 23, 2019
  • KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU 2021 June 10, 2021
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • MBULU DC YATOA SADAKA KITUO CHA AFYA DONGOBESH.

    January 30, 2025
  • MBULU DC YAKWAMUA VIKUNDI VYA VIJANA KIUCHUMI

    February 13, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 38.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZA WANAFUNZI WARIPOTI SHULENI

    January 31, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

MBULU DC KUKUSANYA ZAIDI YA MIL.90 KATIKA MSIMU MPYA WA UVUVI KUTOKA BWAWA LA BONDELA YAEDA CHINI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.