Na, Ruth Kyelula, Mbulu DC.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Abubakar Kuuli, amewataka Wauguzi wote wa Mbulu DC kuwa na lugha nzuri na zenye staha kwa wagonjwa pamoja na wale wanaowasindikiza wagonjwa katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya.
Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu wakati wa maadhimisho ya siku ya Wauguzi Duniani iliyofanyika ki Halmashauri Mei 16, 2025, katika viwanja vya shule ya sekondari, Ufundi na Chuo cha Biblia Stenroos, kilichopo Dongobesh Wilayani Mbulu.
“Ni vyema maadhimisho haya tukayadumisha, kama tulianza kufanya maadhimisho haya kwenye vituo, safari hii tunafanya kama Halmashauri.Hili jambo tunatakiwa tulidumishe. Wale wataokuwa hawako zamu na kama hawatoathiri huduma za afya kwenye vituo vyao, tukutane kwa pamoja tuzungumze.” Alisema Kuuli.
Aidha amewapongeza Wauguzi kwa kufanya sherehe hii kwa mara ya kwanza ki Halmashauri, wakiongozwa na Muuguzi mkuu wa Halmashauri Pellagia Shirima.Na kuongeza kuwa safari hii wauguzi wamejiongeza pakubwa.
Kwa upande wake Mkuu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Neema Aligawesa, alisema kuwa wauguzi ni watu muhimu sana kwa mstakabali wa afya za binadamu na kuongeza kuwa kazi ya uuguzi ni wito, wafanye kazi kwa kuzingatia maadili, miiko, utunzaji wa siri za wagonjwa na lugha za staha.
Naye Muuguzi Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Pellagia Shirima, ametoa wito kwa wauguzi Wote wa Halmashauri ya Wilaya, kufanya kazi kwa kuzingatia utu, heshima na staha, kwahiyo wauguzi wazingatie hayo maadili ya uuguzi.
“Kwa kawaida kila mwaka tunarudia kiapo, tunasema kazi zetu tunafanya kwa miiko na miiko ile kibinadamu huwa tunajisahau kwa hiyo angalau kila mwaka, lazima Muuguzi arudie kile kiapo kukumbuka ile miiko ambayo anatakiwa asifanye wakati wakutoa huduma za kiuuguzi, ndio mana huwa tunakula tena kiapo ili kukumbushana.” Alisema Pellagia.
Vile vile amewataka Wauguzi wafute nyayo za muanzilishi wa Wauguzi Duniani Florence Nightingale alivyoweza kuwahudumia watu wa vita, aliwahudumia kwa busara, heshima na pale hata alipokosa taa aliwasha mshumaa anawaangalia hata gizani, anawaponya yale majeraha kwa upole na staha, na ninyi wauguzi mnanatakiwa kufuata nyayo zile zile muendelee kutoa huduma bora na nzenye heshima.
Mbulu district Coucil
Anuani: P.O.BOX 74
Simu ya mezani: +255743583078
Simu: +255716992222
Barua pepe: md@mbuludc.go.tz
Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.