• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Dinamu
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

MGANGA MKUU WA WILAYA AITAKA JAMII IWAIBUE WATOTO WENYE CHANGAMOTO YA LISHE

Kurushwa hewani: September 26th, 2024

Na, Ruth Kyelula, Mbulu DC

Mganga Mkuu wa Wilaya, Dr. Shadrack Makonda, ameitaka jamii iweze kuwaibua watoto wenye changamoto ya utapiamlo na udumavu kwa kutumia vifaa vya kupima mzingo wa mkono ili kujua mtoto amekonda ama la, kifaa cha kupima udumavu kama ameongezeka urefu ama la na mzani wa kujua uzito wa mtoto.


Mganga mkuu Wilaya,, Dr. Shadrack Makonda, akifungua mafunzo ya Tathimini ya hali ya lishe kwa watoto chini ya miaka mitano. 

Hayo yalisemwa na Mganga mkuu wa Wilaya Dr. Shadrack Makonda wakati akifungua mafunzo ya tathimini ya hali ya lishe kwa watoto chini ya miaka mitano, kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii, yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri September 24,2024.

Mganga Mkuu,Maafisa Lishe na Wahudumu wa afya ngazi ya jamii wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya mafunzo.  

“Lengo ni moja, tuwabaini, tuwagundue watoto wenye changamoto ya lishe ili tuweze kuwasaidia. Kwenye jamii zetu wapo watoto wenye changamoto za lishe, wapo wenye utapiamlo, wapo wenye udumavu, na unakuta mtoto akiwa na changamoto hiyo zipo familia zina mficha. Kwahiyo ninyi ndio wa kuwaibua watoto hao kwa sababu ninyi ndio mnaishi kwenye jamii, mnazijua familia na mnawaona watoto wenye changamoto”. Alisema Dr. Shadrack.

Kwa upande wa Afisa Lishe Wilaya ya Mbulu, Jackline David, amesema kuwa Wahudumu wa afya ngazi ya jamii wamekuwa msaada mkubwa sana kwa kuibua matatizo mbali mbali yanayojitokeza katika jamii ikiwa na pamoja kuwaibua watoto wenye utapiamlo mkali, matukio ya ukatili wa kijinsia yanayoenedelea na shughuli zingine jumuishi.

Aidha Afisa lishe amesema kuwa, elimu wanazozitoa katika jamii zizingatiwe, mfano wanapotoa elimu ya ulaji sahihi wa makundi sita ya chakula lakini pia ameomba washirikiane katika matukio ya kikatili ya kijinsia yanayotokea yasibaki kwenye jamii ili waweze kusaidiana, lakini pia wahudumu wa afya ngazi ya jamii wapewe ushirikiano.

Afisa Lishe wa Wilaya, Jackline David akitoa mafunzo kwa Wahudumu wa afya ngazi ya jamii.  

Naye Afisa Lishe, Lutengano Emmanuel amesema kuwa mafunzo hayo yamefanyika kwa awamu ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2024/2025, na kuhudhuriwa na wahudumu wa afya ngazi ya jamii ishirini na tatu (23).

Lutengano aliendelea kusema kuwa, wahudumu wa afya ngazi ya jamii waendelee kufanya kazi kwa weledi   ili waweze kuibua watoto wengi na kuweza kujua tathimini ya hali ya lishe imefikia katika kiwango gani lakini pia anatoa wito kwa watendaji wa vijiji na kata kushirikiana nao ili tathimini ifanyike kwa ukubwa na uzuri.


Afisa Lishe, Lutengano Emmanuel akitoa mafunzo kwa Wahudumu wa afya ngazi ya jamii.  


Matangazo

  • Tangazo la fursa za mafunzo ya ufundi stadi awamu ya saba February 01, 2025
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • JINSI YA KUTOA/KUTUMA MALALAMIKO KWA NJIA YA MTANDO HALMSHAURI YA WILAYA YA MBULU. March 23, 2019
  • KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU 2021 June 10, 2021
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • MBULU DC YATOA SADAKA KITUO CHA AFYA DONGOBESH.

    January 30, 2025
  • MBULU DC YAKWAMUA VIKUNDI VYA VIJANA KIUCHUMI

    February 13, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 38.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZA WANAFUNZI WARIPOTI SHULENI

    January 31, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

MBULU DC KUKUSANYA ZAIDI YA MIL.90 KATIKA MSIMU MPYA WA UVUVI KUTOKA BWAWA LA BONDELA YAEDA CHINI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.