• Mlalamikaji |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Mbulu District Council
Mbulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Taasisi
    • Orodha ya Wakurugenzi
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya utumishi na mahusiano
      • Mipango, Takwimu na Uangalizi
      • Idara ya Fedha
      • Elimu na Utamaduni
      • Afya
      • Kilimo.Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na uthibiti wa taka ngumu
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Idara ya Ujenzi na Zimamotto
        • Moto
      • Idara ya Maji
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Goverment Communication
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Sheria
    • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Picha Jongefu
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi inayoendela
    • Miradi iliyokamilika
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Dinamu
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Ardhi
      • Kamati ya ALAT
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba za Vikao
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Sekta ya Viwanda
    • Sekta ya Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Elimu

Vifaranga vya Samaki 15,000 Vyapandikizwa Katika Mabwawa 3 Ili Kuongeza Wigo wa Mapato Kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.

Kurushwa hewani: October 19th, 2021

Mtaalamu wa Ufugaji Samaki Kutoka Kampuni ya Aquatel Fish Farming Consultancy Toka Mwanza Bw. Simon C. Akiwa na Furushi la Vifaranga wa Samaki Tayari Kwa Kupandikiza Majini.



Kushoto ni Dereva wa Halmashauri Bw. Budoya

Baada ya Kushushwa Kutoka Kwenye Gari Vifaranga Hao wa Samaki Sato Walipelekwa Hadi Sehemu ya Kupandikiza Bwawa la Dongobesh Kama inavyoonekana.

Aliyevaa Kofia Nyekundu Kushoto ni Afisa Mipango (W) Bw. F. Kundi na Kulia Aliyenyanyua Mikono ni Afisa Mifugo na Uvuvi (W), Bw. Moses Nduligu.


Mtaalamu wa Samaki Bw.Simon C. Saji wa Kampuni ya Aquatel Fish Farming Consultancy Akiwa na Kifaa Maalumu Yaani  kipima joto "Thermometer" cha Kupima Joto la Maji Husika.

Upandikizaji Likiendelea Katika Bwawa la Dongobesh Mbulu.


Hapo Sio Kigamboni Dar es salaam ni Dongobesh - Mbulu, Muonekano wa Bwawa la Dongobesh. 



Huo ni Mfereji wa Umwagiliaji Uliyotengenezwa Kisasa kwa Kuweza Kuyaruhusu Maji Kiasi Kinachotakiwa Kwenda Mashambani. Hao Unaowaona ni Ndege Walao Viumbe vya Majini Waitwao Kurastara, Wanapatikana Hapa Kama Unavyowaona Mpenzi Msomaji.



Mtambo wa Kusukuma Maji Kiasi cha Kilometa 4 Hadi Kufikia Mashamba Husika Ili Katika Kilimo cha Umwagiliaji Kata ya Dongobesh - Mbulu.


Upandikizaji Likiendelea Katika Bwawa la Mangisa.


Muonekano wa Bwawa la Mangisa.






~~~~~~~~~~~        HABARI KAMILI        ~~~~~~~~~~~ 



Katika kuhakikisha Halmashauri inaongeza mapato ya ndani ili kuweza kuongeza nguvu ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kupitia idara ya mifugo na uvuvi watimiza azima ya kupanda vifaranga 15,000 vya samaki aina ya Sato katika mabwawa 3 yaani bwawa la Dongobesh, Mangisa na Muslur tarehe 16.10.2021. Katika kazi Hii kampuni ya Aquatel Fish Farming Consultancy toka Mwanza ndiyo iliyoshida tenda ya upandaji huu ambapo mtaalamu wa Samaki hawa bwana Simon C Saji wa kampuni hiyo alianza kwa kupima joto la maji ya bwawa husika na kifaa maalumu yaani kipima joto "Thermometer" kisha zoezi la kuwapanda ndipo liliendelea.


Kuhusiana na zoezi hili wataalamu hawa walifika miezi kadhaa nyuma kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu juu ya mabwawa haya kwa aina ya maji, joto la nje na ndani ya maji, aina ya vyakula vilivyopo , muelekeo wa maji ulivyo kikondo na uwingi wa maji ya bwawa husika ambapo katika utafiti huo ndiyo uliopelekea kufanya maamuzi ya kupandwa samaki hawa.


Taarifa za wataalamu hawa wamesema samaki hawa watakuwa hadi kufikia wakubwa kwa muda wa miezi 3 ambapo hapo na wao wataanza kujamiiana na kuanza kutaga mayai ambapo baada ya miezi 3 tena samaki watakuwa tayari ni wakubwa na kuanza kuvunwa kwa ajili ya matumizi ya chakula kwa binadamu. Hivyo wananchi wameaswa kutoshiriki katika zoezi lolote la kuvua hadi hapo watakapotangaziwa rasmi kwa lengo la kuweka mazingira wezeshi ya hawa samaki kuzaliana kwa wingi.


Kimsingi samaki pia ni kitoweo tosha kwa wananchi kwa chakula kwa kuongeza protini mwilini inayojenga mwili na kulinda pia, na zoezi la uvuvi litakapokuwepo hapa itaibua biashara nyingi "associative business" kuanzia mama lishe, usafirishaji, vituo vya kuweka na kutoa fedha kwa njia ya mtandao na mengine mengi hivyo ajira kupatikana na kuongeza mzunguko wa kifedha katika maeneo haya na Wilaya kwa ujumla wake. Imefahamika kwamba katika mabwawa haya awali yalikuwa yanatumika katika kilimo cha umwagiliaji wa mimea kama vile vitungu maji, vitunguu swaumu, kariti na mazao mengine ya biashara kazi inayoendelea hadi sasa kwa kutumia mitambo ya kusukuma maji kwa umbali wa hadi kilometa 4.


Haya hayaji tu kutoka hewani bali ni mipango thabiti ya Idara ya husika ya Mifugo, Menejimenti ya wataalamu kwa ushirikiano wa Baraza la madiwani katika lengo kuu la kupata fedha zitakazotatua kero mbalimbali za wananchi.

Matangazo

  • Tangazo la fursa za mafunzo ya ufundi stadi awamu ya saba February 01, 2025
  • TANGAZO LA ZABUNI YA UCHIMBAJI VISIMA January 29, 2019
  • JINSI YA KUTOA/KUTUMA MALALAMIKO KWA NJIA YA MTANDO HALMSHAURI YA WILAYA YA MBULU. March 23, 2019
  • KARIBU MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU 2021 June 10, 2021
  • Tazama zote

Habari za hivi Punde

  • MBULU DC YATOA SADAKA KITUO CHA AFYA DONGOBESH.

    January 30, 2025
  • MBULU DC YAKWAMUA VIKUNDI VYA VIJANA KIUCHUMI

    February 13, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 38.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZA WANAFUNZI WARIPOTI SHULENI

    January 31, 2025
  • Tazama zote

Picha Jongefu

MBULU DC KUKUSANYA ZAIDI YA MIL.90 KATIKA MSIMU MPYA WA UVUVI KUTOKA BWAWA LA BONDELA YAEDA CHINI
Video za Ziada

Viunganishi ya Haraka

  • Facility Financial Accounting and Reporting System(FFARS)
  • Log in PlanRep System
  • PlanRep Documents
  • FFARS USER GUIDE
  • MANYARA REGIONAL WEBSITE
  • UTUMISHI PORTAL

link tunazolandana

  • TOVUTI YA IKULU
  • MFUMO WA VIBALI YA KUSAFIRI NJE (LIVE)
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • BARAZA LA MTIHANI LA TAIFA TANZANIA
  • TOVUTI YA HABARI MAELEZO

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Uelekeo wa Ramani

Wasiliana nasi

    Mbulu district Coucil

    Anuani: P.O.BOX 74

    Simu ya mezani: +255743583078

    Simu: +255716992222

    Barua pepe: md@mbuludc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Awali
    • Kanusho
    • Maswali yanaolizwa Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbulu District Council . All rights reserved.